Kikwete abariki nyongeza ya mishahara
Friday, 22 April 2011 09:41
*asema hatabinafsisha tena TRL, Bandari
RAIS Jakaya Kikwete
Patricia Kimelemeta RAIS Jakaya Kikwete ameahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi kupitia bajeti ya Serikali katika mwaka wa fedha, 2011/2012. Rais Kikweta alitoa ahadi hiyo juzi alipokuwa akizungumza na viongozi wa Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi nchini (Tucta), Ikulu jijini Dar es Salaam . Mkutano baina ya Tucta na Rais ni wa kwanza tangu Kikwete achaguliwe kwa mara ya pili kuongoza nchi katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka jana.
Katika mwaka wake wa mwisho wa ngwe ya kwanza ya uongozi wake, Serikali ya Kikwete iliingia katika malumbano makali kuhusu suala la stahili za wafanyakazi na mishahara midogo iisiyolingana na gharama za maisha.
Naibu Katibu Mkuu wa Tucta, Nicolaus Mgaya aliliambia gazeti hili katika mahojiano maalumu jana kuwa, pamoja na mambo mengine, Rais ameahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi ili kuwapunguzia makali ya maisha. “Mishahara ya wafanyakazi ni midogo, ikilinganishwa na kipindi hiki cha kupanda kwa gharama za maisha. Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete ameihaidi kuongeza mishahara kwenye bajeti hii ya fedha ya mwaka 2011/12,”alisema Mgaya...... kwa taarifa zaidi, ingia kwenye hii source:
Katika mwaka wake wa mwisho wa ngwe ya kwanza ya uongozi wake, Serikali ya Kikwete iliingia katika malumbano makali kuhusu suala la stahili za wafanyakazi na mishahara midogo iisiyolingana na gharama za maisha.
Naibu Katibu Mkuu wa Tucta, Nicolaus Mgaya aliliambia gazeti hili katika mahojiano maalumu jana kuwa, pamoja na mambo mengine, Rais ameahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi ili kuwapunguzia makali ya maisha. “Mishahara ya wafanyakazi ni midogo, ikilinganishwa na kipindi hiki cha kupanda kwa gharama za maisha. Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete ameihaidi kuongeza mishahara kwenye bajeti hii ya fedha ya mwaka 2011/12,”alisema Mgaya.
Nape aonya hakuna fisadi atakayepona
Thursday, 21 April 2011 19:12 newsroom
- Asisitiza agizo la siku 90 lipo palepale
Mr Nape Nnauye
CHAMA Cha Mapinduzi kimesema hakitarudi nyuma wala kukata tamaa katika mkakati wake wa kuwaondoa watuhumiwa wa ufisadi ambao wamepewa miezi mitatu kujitafakari na kujiengua wenyewe. Kimesisitiza kwamba watuhumiwa ambao hawataki kuachia nyadhifa zao kwa hiari, wataondolewa kwa nguvu ya Chama, licha ya kuwatumia baadhi ya wanasiasa, vyombo vya habari na viongozi wa dini kuwachafua viongozi waandamizi wa Chama na kupotosha ukweli.
Kauli hiyo ya CCM imekuja baada ya baadhi vyombo vya habari kuanza kuandika habari za kuwadhoofisha viongozi wa Sekretarieti mpya ya CCM kwa lengo la kupunguza kasi ya utekelezaji wa mikakati ya kuwaondoa watu hao katika nafasi za uongozi. Akizungumza na Uhuru jana, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema kila wanachokisema kwenye mikutano ya kujitambulisha ni maamuzi yaliyopitishwa kwenye vikao vya Chama na si msimamo wa mtu mmoja.
..... kwa taarifa zaidi, ingia kwenye hii source:
Makinda atakiwa kulinda heshima ya Bunge
21st April 2011 @ 23:59
21st April 2011 @ 23:59
Anne Makinda
Na Stella Nyemenohi
KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesema Spika wa Bunge anapaswa kutumia wadhifa wake na kanuni za Bunge kulinda heshima ya Bunge. LHRC imeainisha kasoro zilizojitokeza katika Mkutano wa Tatu wa Bunge la 10 uliomalizika Dodoma Aprili 16. Kituo hicho kimesema kulikuwa na ukiukwaji wa maadili na kanuni za Bunge, kwa baadhi ya wabunge na kusema umefika wakati, Spika atumie mamlaka na kanuni zilizopo, ili wabunge waache kutumia lugha zisizo na staha bungeni.
“Spika atumie mamlaka na kanuni za Bunge ili kudhibiti maudhui, mantiki na maana ya mijadala ya Bunge bila kuathiri maslahi ya taifa … Spika ana dhamana ya kuhakikisha ushabiki wa kisiasa haupati nafasi kuvuruga Bunge,” amesema Kaimu Mkurugenzi wa LHRC, Imelda Urio.
“Spika atumie mamlaka na kanuni za Bunge ili kudhibiti maudhui, mantiki na maana ya mijadala ya Bunge bila kuathiri maslahi ya taifa … Spika ana dhamana ya kuhakikisha ushabiki wa kisiasa haupati nafasi kuvuruga Bunge,” amesema Kaimu Mkurugenzi wa LHRC, Imelda Urio.
..... kwa taarifa zaidi, ingia kwenye hii source:




